Kwa taarifa yako tu, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 18 (3) inasema kwamba:-
"Mtu yeyote hatakuwa na mamlaka ya kusaini Mkataba wa KUKUBALI KUSHINDWA VITA NA KULITOA TAIFA KWA MSHINDI, WALA KURIDHIA KUTAMBUA KITENDO CHA UVAMIZI AU MGAWANYIKO WA JAMHURI YA MUUNGANO AU SEHEMU YOYOTE YA ARDHI YA ENEO LA TAIFA NA BILA KUATHIRI KATIBA HII NA SHERIA ZILIZOWEKWA, hakuna mtu atakayekuwa na haki ya kuwazuia raia wa Jamhuri ya muungano kupigana vita dhidi ya adui yeyote anayeishambulia nchi"
Kwa mantiki hiyo, Kama inabidi kupambana na Malawi basi itakuwa ni mapambano mpaka tone la mwisho,
Kwa kuwa Eneo la Ziwa Nyasa kwa upande wa Tanzania linatambuliwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano, hivyo basi, kuridhia Wamalawi kuingia nchini kwa namna yoyote ile ni kuvunja katiba ya nchi,
Kujaribu kuigawanya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa namna yoyote ni Kuvunja katiba ya nchi.
Halafu mwisho, inapofikia hatua Rais anatangaza Vita na adui yoyote anayeishambulia nchi, HURUHUSIWI KUPIGA KAMPENI ZA KUZUIA, AU KUWAZUIA raia wa taifa hili kupigana vita ni Uhaini....unastahili kunyongwa....
I love my Country Tanzania
MUNGU IBARIKI TANZANIA

No comments:
Post a Comment